[wp1s id=”513″]
Upimaji wa ardhi ni nini?
Upimaji wa ardhi ni mfumo wa kijiografia unaooanisha mchoro wa mipango miji na uhalisia kwa kuzingatia taratibu za makazi bora ili ardhi husika ipate vigezo vya kumilikiwa kisheria.
Faida za Upimaji wa ardhi
Zipo faida nyingi za upimaji ardhi ambazo kila mwenye fikra ni rahisi kuzifikiria na kutambua nyingine zaidi baada ya kusoma zilizoorodheshwa hapa chini :->
1 . Kuipa ardhi thamani halisi ya wakati huo.
2 . Kumiliki ardhi kisheria
3 . Kumaliza migogoro ya ardhi kwa asilimia mia ( 100% )
4 . Kuishi bila hofu ya hasara panapo mabadiliko ya maendeleo ya kitaifa.
5 . Kuitumia rasilimali ardhi kwa maendeleo ya kiuchumi.
6 . Zipo nyingine nyingi hizo ila hizo ndio msingi :>>>>>>>>>>>>>
Namna za Upimaji
( a ) Upimaji Binafsi.
( b ) Upimaji shirikishi.
( a ) Upimaji Binafsi ni kupima ardhi kwa mmiliki wa ardhi mmoja mmoja
( b ) Upimaji shirikishi ni kupima ardhi kwa kuchangia gharama za upimaji baina ya wamiliki wa ardhi
KWA MAHITAJI YA KUPIMIWA ARDHI
WASILIANA NASI

Zip